matukio burudani injili uimbaji maisha sanaa muziki maigizo habari maajabu vichekesho maendeleo mafanikio uchumi lugha maono mahubiri nyimbo biblia siasa

Sep 9, 2013

JOSEPHINE NKILA (MINZA) KUFANYA UZINDUZI WA DVD YAKE MPYA INAYOITWA "MAISHA YA IBADA" TAREHE 22/09/2013 PALE CCC UPANGA...

 

ANGALIA MFANO TU WA VIDEO YA  NYIMBO MOJAWAPO ALIYOIMBA SIKU HIYO YA LIVE RECORDING PALE CCC UPANGA(home library camera)

Ni wewe Bwana 22/05/2011
 

Mwanadada Josephine Nkila (MINZA) ambaye mara nyingi uhudumu na Mwalimu Mgisa Mtebe wa huduma ya Robbon Ministries. Anategemea kuachilia Video yake mpya itakayokuja kwa jina la MAISHA YA IBADA (LIFE OF WORSHIP) tarehe 22 September 2013. Video hiyo ambayo imechukuliwa live katika Ukumbi wa Upanga City Christian Centre, mahali ambapo Video hiyo itazinduliwa hapo hapo pia



Huyu  ndiye Josephine Nkila mtumishi wa Mungu tangu akiwa mtoto mdogo. Kinywa chake kimejaa sifa na tenzi za rohoni. usikose kuja kumuona akiongoza maelfu ya wakazi wa dar es salaam na tanzania pale ccc upanga 22/09/2013 kuanzia saa nane mchana. Njoo mama, mtoto, dada.  babu, bibi, shangazi, mjomba na baba na wengineo....

Record ya kwanza kabisa ilifanywa pia kwa ubora wa hali ya juu.

MAISHA YA IBADA


Hii ni picha kutoka katika video ya kwanza yake josephine nkila ambayo ilijulikana kwa jina la nakuabudu bwana ambayo ilifanya na bado inafanya vizuri sana sokoni kwa kuinua mioyo ya watu na kuwasogeza karibu na Mungu wetu (JEHOVA)


kamati ya maandalizi kazini

Josephine Nkila(MINZA)



 Kama inavyoonekana katika picha hapo chini wakati video hiyo ikirekodiwa, Usikose siku hiyo

 Akishirikiana na wanamuziki wafuatao:
Abednego Hango, Ipyana Kibona, Prisca Kangi, David Yona, Jenifer Mushi na Samuel Yona ambaye ndiye producer aliyeisuka album hiyo.

 Picha kwa hisani ya blog mbalimbali za injili.............

Angalia hizi

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...