matukio burudani injili uimbaji maisha sanaa muziki maigizo habari maajabu vichekesho maendeleo mafanikio uchumi lugha maono mahubiri nyimbo biblia siasa

Feb 1, 2017

ALIONGOZA MITIHANI YA FORM 4 MWAKA 2016 ASEMA HAYA.

Kinara wa Kidato cha Nne Nchini Afichua Siri ya Kufanya Vizuri,Adai ni Mungu na Wazazi Tu..!!!

Mwanafunzi wa kwanza katika matokeo ya kidato cha nne nchini kutoka shule ya Sekondari ya Feza Boys jijini Dar es Salaam, Alfred H. Shauri (katikati) akielelzea siri ya mafanikio yake kwa wanahabari.

MWANAFUNZI wa kwanza kitaifa katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2016, Alfred H. Shauri, ameeleza siri ya mafaniko yake kuwa ilitokana na kusoma kwa bidii na kumtanguliza Mungu katika kila alichofanya.

Akizungumza na wanahabari katika Shule ya Sekondari ya Feza Boys alikosoma eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam, amesema kitu cha  kwanza katika kila alilofanya ni kumtanguliza Mungu katika masomo yake na cha pili alikuwa sambamba na wazazi wake kuhakikisha anachukua ushauri wao juu ya masomo yake ambapo kwa uapnde wa walimu wake alisema aliwasikilza kwa makini na kuwauliza maswali pale alipokuwa akihitaji msaada na kujisomea vitabu mbalimbali.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shule za Sekondari za Feza, Ibrahim Yunus,  alisema kuwa mafaniko ya mwanafunzi huyo yametokana na juhudi zake mwenyewe alizokuwa nazo wakati akiwa shuleni hapo kwani aliweza kuwa wa kwanza pia katika shindano la insha  iliyozikutanisha shule za Afrika Mashariki mwezi Mei mwaka jana.
Source: udakuspecially.com

Angalia hizi

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...